Wednesday, October 30, 2013

TANGANYIKA ONE: WAASI WA M23 WAONDOLEWA NCHINI DRC

TANGANYIKA ONE: WAASI WA M23 WAONDOLEWA NCHINI DRC:



Wanajeshi wa DRC wakishirikiana na jeshi la UN
linaloongozwa na wanajeshi wa Tanzania wamefanikiwa kuwaondoa waasi wa
M23 kutoka katika ngome yao kuu katika eneo la Bunagana mpakani na Uganda
 Mji wa Bunagana umekombolewa
kufuatia makabiliano makali adhuhuri ya jana ambapo baadhi ya waasi
walilazimika kuimbilia msituni huku baadhi yao wakidai waliingia Uganda wakiwa wamevalia mavazi ya kiraia
    
Msemaji wa serikali alisema kuwa mji wa Bunagana ulio katika mpaka wa Uganda na DRC, sasa uko chini ya wanajeshi wa serikali.

 .




Hatua hii ya wanajeshi ni sehemu ya ushindi
mkubwa ambao wanajeshi wamekuwa wakiupata dhidi ya waasi hao wa M23
wanaopambana dhidi ya serikali ya DRC  huku wakidaiwa
kusaidiwa na serikali ya Rwanda.







 Umoja wa Mataifa umesema kuwa wakimbizi elfu tano wamelazimika kutoroka Bunagana na kuingia Uganda kwa usalama wao.

No comments:

Post a Comment