Wanajeshi wa DRC wakishirikiana na jeshi la UN
linaloongozwa na wanajeshi wa Tanzania wamefanikiwa kuwaondoa waasi wa
M23 kutoka katika ngome yao kuu katika eneo la Bunagana mpakani na Uganda
linaloongozwa na wanajeshi wa Tanzania wamefanikiwa kuwaondoa waasi wa
M23 kutoka katika ngome yao kuu katika eneo la Bunagana mpakani na Uganda
Mji wa Bunagana umekombolewa
kufuatia makabiliano makali adhuhuri ya jana ambapo baadhi ya waasi
walilazimika kuimbilia msituni huku baadhi yao wakidai waliingia Uganda wakiwa wamevalia mavazi ya kiraia
kufuatia makabiliano makali adhuhuri ya jana ambapo baadhi ya waasi
walilazimika kuimbilia msituni huku baadhi yao wakidai waliingia Uganda wakiwa wamevalia mavazi ya kiraia
.
Hatua hii ya wanajeshi ni sehemu ya ushindi
mkubwa ambao wanajeshi wamekuwa wakiupata dhidi ya waasi hao wa M23
wanaopambana dhidi ya serikali ya DRC huku wakidaiwa
kusaidiwa na serikali ya Rwanda.
Umoja wa Mataifa umesema kuwa wakimbizi elfu tano wamelazimika kutoroka Bunagana na kuingia Uganda kwa usalama wao.